Friday, January 30, 2009

Na hili je?

Unapoletewa maji kama haya je mara zote unakuwa na uhakika yanapotoka?
Au tunaangalia shida ilivyotubana tu...?

Cheka Kiafya!!

Add ImageKuna sehemu moja Mkoani Mtwara inaitwa Nakapanya na ingine inaitwa Nanguruwe, hii ni kweli na ucheke kiafya tu sio sana. Kuna dada mmoja wakati mahojiano yakiendelea kuhusu maisha yake nk, nk, ilifika kipindi katika maelezo yake ilikuwa hivi:
...mimi niliolewa Nakapanya nikaachika nikaenda kuishi Nanguruwe...
Yaani akimaanisha aliwahi ishi maisha ya ndoa Nakapanya na baadae akaenda kuishi Nanguruwe.
Ni story ya kweli si ya kutunga.
Kiafya tafadhali!

Ni mapambo tu sio wa ukweli.

Anaweza kuwa kivutio kama ni nyumbani kwako, garden nk nk.



Usafiri wetu kijijini ndio huooo!!

Hali ndio kama hivyo pichani, ukikosa Land Rover almaarufu Muhogo basi utapanda Kenta ama Lori. Ya mjini mjini na kijijini kijijini tu.

Hali halisi kipindi cha mvua...

Watoto hawa nimewakuta wakicheza kwenye maji yaliyotuama ya mvua. Yawezekana shida ya maji vijijini hufanya mpaka hali kama hii ikitokea watoto hawa husherekea. Na wazazi wao sio kwamba walikuwa mbali na watoto hao? Hapana.
Huyu ndie nisema kama kwenye swimming pool basi ndio yupo deep.
Vijimamboz hivyo na patastories.


Mambo yanapokwenda mrama!


Tairi la Lori aina ya fuso likiwa limechomoka na kubakiza nafasi ya fundi kuja kupata ugali wa watoto. Sijajua ni mzigo ulikuwa mzito ama vipi?

Ujenzi huu wa bila mifereji ya maji???

Pichani ni kwamba mkandarasi alipewa kipande cha kukikarabati, lakini kiukweli mifereji ja maji hamna na ndio sababau ya hali kama hiyo pichani. Comment!!

Ukweli kuhusu Prison Break

Prison Break

Ukweli kuhusu Prison Break, imezoeleka masikioni na machoni mwa wengi kuona mitaani Prison Break inapatikana mpaka season eight (8). Hii nathibitisha wazi kuwa Prison Break kihalisia haijafika season eight (8). Hizi mnazoziona mitani ni Episodes tu toka season halali season four (4).

Kwa wanaofuatilia kwa makini watajua ninamaanisha nini. Ukweli ni kwamba kibiashara tu ili kupata pesa wadau Fulani fulani ili wasilale njaa ndio wameamua kuikata kata vipande “episodes” hizo na kuzigawanya katika mafungu wayajuayo wenyewe na kuyaita “season Fulani mpaka Fulani. Ukweli unabaki pale pale kuwa wananchi wamekuwa wakinunua season moja mara nne zaidi bila wao kujua. Ila kutokana na utamu wa sinema yenyewe then watu kwao ni sawa tu bora kuona.

Ilikuwa ni katika kupeana dodoso tu habari ndio hiyo ipo nje nje.