Friday, January 23, 2009

Rift Valley

Hili ndio Bonde la Ufa linavyoonekana kwa juu.

Kanisa Katoliki Mtwara


Samaki Choma


Mkwawa!

Huyu ndiye Mkwawa pichani.

Momonyoko!

Ni moja ya maeneo huko mkoani Iringa.

Mbao kiwandani




Moja ya kiwanda mkoani Iringa.

Ujumbe

Meseji imefika.

Teknolojia


Pichani ni mashine ya kubangulia karanga tayari kwa kuzipeleka sokoni.

Vocation and tour!!

Ndani ya beach ya maraha Msimbati (Mtwara).

Bunju


Samaki huyu anajulikana kwa jina la Bunju, amejaa miba mwili mzima.

Kuku na lift


Radio


Radio hii inahitaji upige handling ndio ianze kuzungumza, hii imetulia kweli kweli.

Mbwembwe!

Mbwembwe zinapochukua mkondo wake.

David Livingstone

Huyu ndio David Livingstone.

Biashara kijijini

Wenye uwezo kijijini hawako nyuma kuinua uchumi kwa namna moja ama nyingine.

Gereji


Kazi ni Kazi

Mkono uende kinywani!

Mtwara City Center

Almaarufu madukani.

Daraja la Umoja




Daraja kiungo baina ya nchi mbili Tanzania na Msumbiji linalopita juu ya mto Ruvuma likiwa linaendelea kujengwa, pichani ni maendeleo yalipo mpaka januari hii ya mwaka 2009.


Trekta mtoto

Teknolojia inabadilika badilika kila kukicha.

Taifa la Kesho

Nikiwa pamoja na taifa la baadae kama si la kesho katika picha ya pamoja.

Mnarani

Mnara almaarufu mnarani Mkoani Mtwara. Nembo ya mapambano dhidi ya Ukimwi ikimwaga meseji kwa kila apitae kwamba ukimwi upo nk nk...

Utaalamu mchangani!!

Pichani utaona weusi weusi, huo ni utaalamu uliosukiwa na kutandazwa chini material aina ya mpira kuepusha magari yapitayo kutokukwama mchangani. Kwa waliowahi kufika Msimbati (mtwara) si pageni kwao, ni karibu kabisa na inapozalishwa gesi izalishayo umeme, na kuna beach almaarufu msimbati.

Vocation!!

Nikiwa na Ndugu yangu (Francis) on vocation Dar mpaka Moro.

Kanisa kongwe!

Hili ni moja ya makanisa ya zamani sana, wanaotoka pande za ifakara watakuwa wanaufahamu zaidi. Tembelea ifakara usafishe macho na kikwangua anga hicho.

Foleni

Msongamano usiku.

Hii ni Imani au Baraka?

Nimebahatika kuona pindi niwapo katika mizunguko yango ya kila siku vijijini kwa gari na kushuhudia nyuma baada ya kupita kwa baadhi ya wanavijiji huchukua wanao wadogo na kwenda kuwakanyagisha zilipoacha/pita alama za matairi ya gari. Nimeshindwa kujua bado mpaka sasa ni nini maana yake!?
Wewe una ufahamu wowote juu ya hili?

Mzani!!

Nilibahatika siku moja kukuta Nurse akisisitiza kwa akina mama kuja na kikalio kama kionekanacho pichani kwa ajili ya kupimia uzito watoto. Nurse huyo aliwaomba akina mama kushonesha kila mtu chake kuepuka kuambukizana magonjwa ya ngozi kati ya mtoto mmoja kwenda kwa mwingine. Kwa kweli nilifurahishwa na hilo hope pia wewe utasambaza elimu hii kwa jamii iliyokuzunguka.

Kisima!

Uvunaji wa maji ya mvua umekuwa njia mbadala sana ya kuepuka shida ya maji katika maeneo mengi vijijini, cha kuvutia visima vingi vimejengewa kwa juu kuzuia watoto wadogo kuweza kuhatarisha maisha yao.

Paradise Hotel

Moja ya hotel inayovutia ndani ya mji wa Bagamoyo Paradise Hotel.

Vocation!!

Vocation pande za Babu na Bibi mara moja moja kwa mwaka.

Pool table bush

Hii nimeifuma mwaka huu mwanzoni.
Hii niliifuma mwaka jana mwishoni, mambo ya vijijini hayo hawapo nyuma.

Teknolojia

Moja ya Gari la aina yake (Cadillac) lenye kutumia mafuta ya Nuclear.

Maoni mtini!

Moja ya style ya pekee boxi la maoni kuning'inia mtini, swali je kipindi cha mvua inakuwaje hapo?

Mwelekaz

Pindi mzigo unapoelemea upande mmoja wakati wa kunesa nesa hali huwa hivi pichani.

Bilicana

Bilicana ya pande zileee.

Solar power

Nishati ya umeme itumiayo mionzi ya jua imekuwa ikitumika sana maeneo ya vijijini, pamoja na hayo miradi mbali mbali ya kimataifa imekuwa ikiwezesha kwa baadhi ya zahaniti na vituo vya afya ikiwa ni pamoja na nyumba za wahudumu kuopata huduma ya umeme huu.

Kimbunga

Pindi kimbunga kipitapo hali huwa hivi...

Mnara Kileleni

Mnara mmoja wapo wa simu za mikononi uliojengwa juu ya mwamba mgumu.


Hali halisi

Maji ya kuoga katika moja ya Guest House moja ndani ya wilaya fulani, hali hii huna budi kukubaliana na matokeo maana maji ndio hayoo toka kisimani.
Pichani uonacho ndio key holder ya guest husika, mwenye guest house anamiliki pikipiki mbili na hela yaingia kila kukicha lakini pichani unajioeaa moja ya key holder ya Guest house yake.


Ifakara Kumekucha




Alamaarufu Mbega Resort ndani ya ifakara (Morogoro), Ukumbi wa mikutano ukiwemo na vyumba vya kulala vyenye kipupwe (Air Condition) vyoote.